SOMO: KUTOKA
UTANGULIZI
Kutoka ni kuhama kutoka nafasi ya chini au kutokuwepo mazingira
ya kwanza kwenda mbele. Mfano unaweza kwenda kwa mtu au kwa rafiki yako usipomkuta
utaamua kuulizia aliko watu watakujibu unayemtafuta hayupo katoka,maana yake mazingira
hayo hayupo.
Nilipokuwa ninasoma habariza wana wa Israeli walipokuwa wako utumwani
Misri Mungu baada ya kuwaona wanateseka sana kwa kutumikishwa na Wamisri aliandaa
mpangowakuwatoa Inchi ya Misri ilikuwapeleka Inchi ya ahadi. Si rahisi kuelewa hali
hii lakini pia mtumishi wa Mungu IBRAHIM
Mungu alipotaka kumuinua na kumbariki awe taifa kubwa ambacho Mungua likifanya
nikumwambia atoke katika Nchi ya baba yake na jamaa yake ili aende mahali atakapo
ambiwa na Mungu, hiyo haitoshi baada ya Yesu kuja Duniani kwa mpango wa kumwokoa
mwanadamua liwakuta kina Petro wakivua samakia lichokifanya nikuwatoa kwenye uvuvi
wa samaki kuwaandaa ili wawe wavuvi wa watu. Swali je kwa nini Yesu asingewapa maagizo
ya kuhubiri mpaka awatoe mahali walipokuwa ndipo aweze kuwapa maagizo? Au
kwanini Abraham hakubarikiwa mpaka alipotoka kwenye Nchi ile? Kumbe tunagundua kutoka
ni kwamuhimu kwa kila mtu. Fikilia juu ya mtoto anapozaliwa anabebwa kwa kuhurumiwa
hata aliyembeba anadhani animuumiza lakini unafikia wakati ambao mtoto atakaa mwenyewe,
ataanza kutambaa. Kusimama, Kutembea hatimaye kukimbia hizo zote ni hatua za kutoka
kwa mtu.
KWA NINI TUNAPASWA
KUTOKA
Kwa nini tunapaswa kutoka?
1.Kwasababu ni mpango wa Mungu. Ili Mungu afanye kazi na
mtu lazima amtoe kwenye mazingira aliyomo, ndipo anapoanza kumtumia kwa mfano ukitizama
katika maandiko matakatifu katika kitabu cha wakolosai inaeleza waziwazi juu ya
swala hili la mtu kutoka katika mazingira au mahali Fulani ili Mungu amtumie
vile apendavyo.
Kol 1:13 ( naye alituokoa
katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa mwana wa
pendo lake.)
Mfano mzuri tuna uona kwa Abraham mwanzo 12:1-2 kabla Mungu hajambariki sharti
la kwanza alilompa alimwambia atoke kwao mahali pa wazazi wake na ndipo alipoanza
kusema naye baada ya kutoka.
2.Ili
kuliondoa tegemeo letu kwa watu au kwa vitu badala yake tumtegemee Mungu Yer 17:5b amelaaniwa mtu Yule amtegemeaye mwanadamu
kusudi la Mungu kumtoa Abraham kwenye nyumba ya baba yake na ya jamaa zake ilikuwa
ni kulivunja tegemeo la Abraham kwa wazazi wake na ndugu zake .
Pointi ya msingi kijana anapokuwa yungali kwa baba yake na
mama yake anakula, anavishwa na kila kitu akiomba anapewa hawezi kuwa na mwamko
wa kimaisha wa kutafuta vya kwake maana tegemeo lake lingalopo kwa wazazi wake
na ndugu zake na mara nyingi vijana wa namna hii hujikuta wakitumia muda wao vijiweni
na vijana wa makundi lika na mwisho kuondokewa na wito wa kiutumishi na kuonekana
mzigo kwa wazazi wao na ndugu zao hadi imepelekea wazazi wao kuwafukuza nyumbani
ili waweze kujitegemea.
ILI UTOKE LAZIMA UYACHOKE MAZINGIRA
ULIYOPO
Mara nyingi
kutokuyachoka mazingira kumewafanya watu
wengi washindwe kutoka mahali walipo mfano huwezi kujenga nyumba au kutoka kwenye
upangaji kama mazingira ya upangaji hayajakuchosha, wapo watu si kwamba hawana pesa
za kuweza kujenga kwao na bado wako katika upangaji, hao mazingira ya upangaji hayajawachosha.
Pia wapo
watu wameshindwa kumtumikia Mungu kwa wito aliowaitia kwa sababu bado wanapenda kuwa washilika kwa hiyo wanajihesabu bado watoto
yer 1:6 yeremia alisema hawezi kuifanya
kazi ya bwana kwa sababu yeye ni motto.
Kutamani
ya kwako mwenyewe hata kama umeajiliwa kwenye kampuni, ofisini au dereva wa daladala
nk. Kama hujatamani kuona kwamba unafanya kazi yako mwenyewe hauwezi kutoka hapo,
tuanmwona yakobo katika mwanzo30:30c alipomtumikia
mjomba yake ilifika kipindi alipomwambia nilini nitaangalia mambo yangu mwenyewe.
Musa
alipokuwa mtu mzima alikataa kuitwa mwana wa binti farao ebr 11:24, kuna hali zingine haziondoki maishani mwa mtu mpaka ajitambue
yeye ni nani na achukue hatua za kukataa hali hiyo kwa jina la Yesu ndipo aweze
kutoka. Shida inakuja kwa mtu asiyejitambua itakuwa kwake vigumu kutoka mahali alipokwenda
mahali pengine.
Mungu anapotaka
kukutumia haangalii sababu za wewe kutokutoka
hapo ulipo na kwenda katika nafasi au daraja ambalo anataka utumike ili kulitimiza
kusudi lake mfano mzuri ni wakati Yeremia anaitwa na Mungu ili aweze kulitimiza
kusudi la Mungu alijitetea kuwa ana umri mdogo lakini Bwana hakuangalia umri au
sababu za Yeremia alichokiangalia ni Yeremia kutimiza kusudi la Mungu yer 1:6-7
Ili
utoke ni lazima kuyaacha mambo Fulani uliyoyazoea Daudi aliambiwa kuviacha vyombo
alivyokuwa navyo ili aweze kulitimiza kusudi la Israeli 1 samweli 17:20,22
Kuna
watu wameshindwa kuitikia kwenye kusudi kwa
sababu ya kutokuacha yale waliyokuwa wameyazoea. Mfano mke wa ruthu kilichomfanya
abaki pale na kuwa nguzo ya chumvi ni kwa sababu ya maisha yaanasa aliyokuwa ameyazoea mwanzo 19:26.
KUUJUA WAKATI WAKO
Mhubiri
3:1 kwa kila jambo kuna majira yake na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu. Onyo usitoke kama wakati wako bado lakini
pia usipishane na wakati wako utakuja kuutafuta hauta upata tena maana utakuwa ni
wakati wa wengine.
Mfano msichana
akishindwa kuujua wakati wa kuolewa atakuwa anatoa majibu kwa wachumba wanao kuja kumchumbia kwamba Mungu hajasema nae kwanini?
1.Anajiona mtoto
2.kutojua kuwa ni wakati wake
3.Kuwalinganisha wachumba wanakuja kumchumbia
i)Elimu
ii)Mwonekano
iii)Mali
Vitu hivi
vimewafanya wasichana wengi kupishana na wakati wa kuolewa, si kwamba ambao wametimiza
umri wakuolewa lakini hawaolewi si kwamba hawajawahi kuchumbiwa lakini walichengana
na wakati hawakujitambua au kujua wakati wao.
Huwezi
kupishana na wakati wako ukaja kupata kivyepesi mpaka ujute. Ombi langu baada ya
kulisoma somo hili Mungu akupe macho ya kuona wakati wako kwa jina la YESU;
ubarikiwe na Bwana AMEN.
Imetayarishwa
na Mwl MUSSA FESTO
Kwa ushauri
au mashauri wasiliana kwa namba hii.
0675415262
No comments:
Post a Comment